Johari: Upofu wa kwenye Filamu ulinitesa
Alianza kuigiza tangu enzi za kundi la sanaa za maigizo la Kaole, lakini hajawahi kushuka kiwango katika uigizaji.
Huyo ni Blandina Chagula maarufu Johari, ambaye 
mbali ya kuigiza amejaliwa kipaji akimudu vyema kuuvaa uhusika katika 
uigizaji na kuonyesha tofauti kati ya huzuni na furaha.
Katika mahojiano yake na Starehe, Johari anaeleza 
mambo mbalimbali asiyoweza kuyasahau katika uigizaji wake ikiwamo 
kulibadili soko la filamu kutoka enzi za kutazamwa bure kupitia runinga 
na sasa kuuzwa kwa wananchi.
Mkali huyo wa filamu anasema kuwa hataisahau tamthilia ya Johari, iliyobeba umaarufu na kumpa jina la usanii ‘Johari’.
Anasema anaikumbuka tamthilia hiyo kwa kuwa ndiyo 
iliyowapa wazo la kubadili mfumo wao wa utendaji kazi kutoka tamthilia 
walizokuwa wakiigiza na kuonyeshwa bure kwenye runinga na kuigeuza kuwa 
biashara, ambapo badala ya shabiki kuvizia vipindi vya televisheni ili 
aitazame vipande vipande, ataipata yote kwa kulipia akinunua Dvd.
“Ilikuwa ngumu sana, lakini kwa kuwa tulikuwa watu
 makini akiwamo marehemu Steven Kanumba, msimamo ulikuwa huo. Kwa shida 
mfumo huo ukakubalika na unafanya kazi vizuri hadi sasa na kuwapatia 
mafanikio wasanii wa filamu kwa kiasi fulani, “anasema.
Johari anaitaja filamu iliyompa shida wakati wa 
kuitayarisha kuwa ni ‘Yellow Banana’, ambapo aliigiza kama mlemavu 
asiyeona (kipofu), huku ukweli akiwa anaona.
Anasema kuwa wakati wa kupiga picha za filamu hiyo
 alipata wakati mgumu kwa kuwa kuna eneo, Vicent Kigosi (Ray), 
aliyeigiza kama mumewe alimpiga kibao huku akitakiwa kutoonyesha kama 
alikuwa anauona mkono uliokuwa ukija kumpiga, wakati ukweli ni kwamba 
aliuona.
Johari anafafanua kuwa jambo jingine 
analolikumbuka katika filamu hiyo ni pale alipoanguka kwenye ngazi, huku
 Ray (mumewe), akiwa amekaa na kimada kwenye kochi.
Anaeleza kuwa kipande hicho kilikuwa kikimliza 
hata akiwa peke yake kwani alianguka kweli hadi ngazi ya mwisho huku Ray
 akimudu vyema kumtazama bila kushtuka kwa kuwa alilewa kwenye penzi la 
kimada, baada ya yeye kuwa kipofu.
“Nilipata shida sana, kila anapotaka kunipiga 
nakwepa, hivyo ilinichukua muda sana kufanikiwa kupata picha isiyokuwa 
na chembe ya mshtuko. Lakini nilipoanguka kwenye ngazi na Ray kutulia 
bila kushtuka. Roho iliniuma kama kweli, hata nilipokuwa nikilia, 
nililia kwa hisia za kweli,” anasema Johari.
Anaeleza kuwa mbali na waigizaji kujituma kuna mambo yanayokatisha tamaa katika uigizaji.
www.2dayhabari.blogspot.com
www.2dayhabari.blogspot.com
0 comments: