MCHEPUKO SI NDIYO DILI, KWA NINI UWE UPANDE MMOJA!
Anayechepuka anaamini kwamba anafanya tendo la siri. Anaamini ni siri yake hivyo si rahisi kwa mwenzake…
Anayechepuka anaamini kwamba anafanya tendo la siri. Anaamini ni siri yake hivyo si rahisi kwa mwenzake kuweza kushtukia mchezo. Tatizo hilo liko katika pande zote mbili japo ukubwa na athari zake zinatofautiana.
Uchepukaji wa mwanamke ni tofauti na ule wa mwanaume. Mwanamke ili achepuke anahitaji muda mrefu kujishauri kabla hajachepuka. Hakurupuki kuchukua uamuzi wa kuchepuka ndiyo maana anahitaji mtu wa kumshawishi sana ili aweze kuchepuka.
Tofauti na mwanamke, mwanaume yeye huligeuza suala la kuchepuka kama ni halali yake. Mara nyingi wanaume huwa wanaamini kuchepuka ni halali yao. Hawachukui muda mrefu sana kujishauri kuingia kwenye mchepuko. Anamuona mwanamke, haraka tu anachepuka.
Wanaume wanaamini kwamba wanapochepuka hawawezi kushtukiwa haraka. Wanaamini kitendo kile watakifanya kwa siri na umakini mkubwa ili wake zao wasiweze kugundua janja yao. Kutokana na kujiamini na kujipa taito ya kuwa mwanaume ndiyo kichwa cha familia, ndiyo maana wengi wanahalalisha tendo hilo na kulifanya eti liwe la kawaida kwa wanaume.
Wanakilainisha kwa maana kwamba wanaweza kuchepuka, wao ndiyo wenye majukumu ya kulea familia. Wanaongozwa na tamaa ya miili hususan kwa vibinti vidogovidogo ambavyo vinahamasisha kwa mavazi, shepu na muonekano wao kwa jumla.
Wanachepuka kwa madai kwamba wapate ladha tofauti. Eti anapokutana na kibinti kidogodogo kinamfanya aweze kuinjoi zaidi kwa sababu anakutana na vionjo vipya. Leo ataanza na huyu, kesho atakutana na mwingine ataonja ladha mpya kesho tena atahamia kwa mwingine.
Tabia inazidi kukua, haimchukui muda suala la kuchepuka kwake linakuwa ni mazoea. Haridhiki kabisa na uwepo wa mkewe peke yake. Hawezi tena kubaki njia kuu, kila siku ataendelea kuchepuka tena akiamini kwa kuwa mkewe hashtukii basi kwa upande wake ni halali lakini si kwa mkewe.
Hoja ya msingi ya kujiuliza hapa ni moja, kama mwanaume ameamua kuchepuka, siku mwanamke naye akichepuka itakuwaje? Kwa nini uamini kwamba mchepuko ni wa upande mmoja na si wa pande zote mbili? Utamu anaoupata mwanaume katika mchepuko ndiyo huohuo unaoweza kumpoza.
Itaendelea wiki ijayo!
0 comments: