Thursday, September 11, 2014

HUKUMU YA OSCAR PISTORIUS YAENDELEA

Oscar Pistorius akiwa amesimama ndani ya mahakama jijini Pretoria baada ya Jaji Thokosile Masipa kuwasili kwa ajili ya kusoma hukumu.
Oscar Pistorius  akisikiliza hukumu yake.…
Oscar Pistorius akiwa amesimama ndani ya mahakama jijini Pretoria baada ya Jaji Thokosile Masipa kuwasili kwa ajili ya kusoma hukumu.
Oscar Pistorius  akisikiliza hukumu yake.
Pistorius akiwa amezungukwa na walinzi, polisi, wanahabari na mashabiki wake wakati akiwasili mahakamani.
Kaka wa Pistorius, Carl Pistorius akiwasili mahakamani akiwa katika baiskeli baada ya kuumua vibaya katika ajali ya gari mwanzoni mwa mwaka huu.
Mama mzazi wa Reeva Steenkamp, June (wa pili kulia) akiwa na baba wa marehemu Reeva, Barry Steenkamp (kulia) wakati wakiwasili katika Mahakama Kuu jijini Pretoria.
Baba mzazi wa Oscar, Henke Pistorius akiwasili mahakamani.
Jaji Thokozile Masipa akipitia majumuisho ya kesi ya mwanariadha Oscar Pistorius kabla ya kutoa hukumu.
Picha hii inaonyesha damu zikiwa zimetapakaa chooni kwa Pistorius baada ya kumpiga risasi mpenzi wake Reeva Steenkamp siku ya Wapendanao mwaka jana. Kulia ni bastora aliyotumia mwanariadha huyo.
HUKUMU ya mwanariadha mwenye ulemavu wa miguu, Oscar Pistorius wa nchini Afrika Kusini inaendelea kwa sasa katika Mahakama Kuu jijini Pretoria.
Hukumu hiyo inasomwa na Jaji Thokozile Masipa ambapo iwapo itabainika kuwa alimuua makusudi mpenzi wake Reeva Steenkamp anaweza kuhukumiwa kifungo cha miaka 25 jela.
Miongoni mwa waliohudhuria hukumu hiyo ni upande wa marehemu Reeva ambapo yupo mama yake mzazi, June na baba yake Barry huku upande wa Pistorius akiwepo baba yake Henke Pistorius, kaka yake  Carl Pistorius aliyepata ajali mwanzoni mwa mwaka huu na kuumia vibaya pamoja na wengineo.
Mapitio ya hukumu hiyo yameanza kusomwa majira ya saa 3: 30 leo asubuhi na bado yanaendelea.

0 comments: