WATU WATATU WANUSURIKA KUFA KWA AJALI DAR
Watu wawili akiwemo raia wa China na dereva ambaye ni mtanzania wamenusurika kufa katika ajali iliyotokea maeneo ya Millennium Tower, Kijitonyama jijini Dar es Salaam ikihusisha gari ndogo aina ya Opa.
Mashuhuda wa ajali hiyo wamesema chanzo cha ajali hiyo ni gari la zimamoto lililokuwa linatokea njia ya Mikocheni kuingia barabara kubwa.
“Gari la fire lilikuwa kasi sana huku likipiga king’ora, kwa hiyo kujihami dereva mwenye Opa akajikuta ameingia mtaroni, tunashukuru hakuna aliyeumia,’’ alisema Robert.
Aidha mtu mwingine aliyenusurika katika ajali hiyo ni Abdukarim ambaye alikuwa ndani ya mtaro huo akisafisha. Kamera ya GPL ilishuhudia askari wa usalama barabarani akiwa eneo la tukio huku break down likianza kuitoa gari hiyo mtaroni.
0 comments: