OBAMA AONYA KUHUSU MKWAMO WA BAJETI

Washington. Rais wa Marekani, Barack Obama amewataka wabunge wa Chama cha Republican waache vitisho na wapitishe bajeti ili kukomesha kufungwa kwa shughuli za Serikali.
Ombi hilo la Obama limekuja wakati baadhi ya
wafanyakazi wa Mpango wa Huduma ya Bima ya Taifa ya Afya wakiendelea
kulalamika kwamba huduma hizo zitaendelea kukabiliwa na matatizo kwa
miezi kadhaa ijayo, kutokana na kutokuwepo kwa huduma za tovuti ya
mpango huo.
Katika hotuba yake iliyoonyeshwa moja kwa moja
kwenye televisheni, Obama ameonya kushindwa kwa Marekani kulipa madeni
yake huenda kukasababisha athari na kuwahimiza wabunge wa Chama cha
Republican kuongeza bila masharti kiwango cha fedha ambazo taifa
linaweza kukopa.
Rais Obama amewaambia waandishi wa habari kwamba
hakuna anayepaswa kuzuiliwa mateka katika kutekeleza mpango huo muhimu
kwa raia wote wa Marekani bila kujali itikadi za vyama vyao.
Obama pia alisema kama Bunge litakataa kukiongeza
kiwango hicho, Marekani haitaweza kugharimia shughuli zake zote kifedha
kufikia katikati ya mwezi huu.
www.2dayhabari.blogspot.com
www.2dayhabari.blogspot.com
0 comments: