MIAKA 18 YA KIFO CHA TUPCA WASANII MMEJIFUNZA NINI?

Tupac Amaru Shakur
Kwa ufupi
Anaitwa Tupac Amaru Shakur, mwanahipop aliyefariki
dunia akiwa na umri mdogo wa miaka 25 ambaye mpaka leo bado dunia
inamkumbuka, na mashairi yake yakitumika katika vyuo mbalimbali
kufundisha falsafa ya kisasa, huku wengine wakimtumia kama mfano wa
kuigwa kutokana na mashairi yake ya kupinga ubaguzi na kuburudisha
wakati mwingine.
Anaitwa Tupac Amaru Shakur, mwanahipop aliyefariki
dunia akiwa na umri mdogo wa miaka 25 ambaye mpaka leo bado dunia
inamkumbuka, na mashairi yake yakitumika katika vyuo mbalimbali
kufundisha falsafa ya kisasa, huku wengine wakimtumia kama mfano wa
kuigwa kutokana na mashairi yake ya kupinga ubaguzi na kuburudisha
wakati mwingine.
Ukiachana na ukorofi wake na mambo mbalimbali
ambayo hayakupendeza kwa jamii bado dunia inamlilia kwa jinsi alivyoweza
kuleta changamoto na mwamko kwenye muziki huo wa kizazi kipya, mpaka
ukapata umaarufu mkubwa duniani.
Hapa ndipo kiuhalisia tunapata mshangao kwamba
mara nyingi mtu huyu alikuwa mkorofi mkorofi, lakini leo dunia ya sanaa
inasimama dakika moja na kumkumbuka kwa jema moja tu, changamoto katika
muziki wa kizazi kipya.
Baada ya kuliona hilo tunarudi tena kwenye tasnia
yetu ya muziki wa kizazi kipya hapa nchini, sijui wana Hip Pop wetu
wamejifunza nini na wao siku wakiondoka tutajifunza nini kutokana na
sanaa yao?
Wasanii wetu, kwa kweli bado ni watu ambao wenyewe
kama walivyo hawana ile nguvu ya kuamua jambo kwa mmoja, mmoja kwa
manufaa ya wengi au kuanzisha msukumo fulani ambao kila mtu akiuona
atatamani kuwa kama yeye, ni wachache sana.
Sasa hivi ukiuliza msanii aliyejiweka kwenye
nafasi nzuri utatajiwa AY aliyejianzishia miradi mingi ambayo kila mtu
anatamani kuwa kama yeye, huku akiamini ameanzisha bila kujihusisha na
kashfa, yoyote na ameweza kupenya kwenye mipaka ya nchi mbalimbali
kufikisha muziki wake.
Wanaharakati walikuwepo lakini baada ya kufanikiwa
kwa jitihada binafsi, harakati wameziweka pembeni na kuwaacha wa chini
ambao walikuwa wakiendelea kutaabika mpaka wengine wameamua kujishusha
na kuomba misamaha kwa wale waliokuwa wakiwashutumu kuwaonea.
Hii ni alama tosha inayotuthibitishia kwamba bado
wasanii wa nyumbani wana safari ndefu kisanii na kimafanikio, na sababu
kubwa ya msingi inayokwamisha maendeleo yao yote hayo ya aina mbili ni
kutokana na kutotambua hasa wanataka nini.
Wasanii wetu wamekosa misimamo katika viwango vya
kazi zao kuanzia kwenye kulipwa mpaka kwenye utengenezwaji wake. Utakuta
wasanii wawili wanafanya muziki wa aina moja, lakini huyu analipwa 10,
huyu analipwa tano na maisha yanaenda.
Mpaka leo wasanii wetu wanaweza kutishwa na kituo
kimoja cha redio kwa kuambiwa ‘hatupigi nyimbo zenu’ na wakaogopa kiasi
cha kupiga magoti huku wakijua dhahiri kwamba ili kituo kifanye kazi
zake kwa ufanisi kinahitaji nyimbo za wasanii.
Kuna kitu cha kujifunza sasa kwa Tupac ambacho
tungetamani wasanii wetu wakijue kinaitwa misimamo, waepukwe kuendeshwa
kama magari mabovu, wawe na uamuzi wao ili kesho na keshokutwa, kuwe na
msingi kwa ajili ya wasanii wanaokuja.
www.2dayhabari.blogspot.com
www.2dayhabari.blogspot.com
0 comments: